[1] Hii ni hoja ya nguvu zaidi katika kubatilisha yale wanayosema Wakristo na Wayahudi kwamba wao ni wana wa Mwenyezi Mungu. Nayo ni kwamba mwana wa Mwenyezi Mungu hana dhambi hata moja; mbali na kuadhibiwa kwayo; kwa sababu mwana huwa wa aina moja na baba yake. Na kwa sababu wao huadhibiwa kwa madhambi yao, basi wao si wana wa Mwenyezi Mungu. (Nadhm Addurar, cha Albaqaaii)