Sema: Mwenyezi Mungu hukuokoeni kutoka hayo, na kutoka kila mashaka, na kisha nyinyi mnamshirikisha!
Sema: Ni Allah, Mwenyezi Mungu wa pekee, ndiye aliye kuokoeni na vitisho hivi, na kila shida nyengineyo. Na kisha nyinyi pamoja na hayo mnamshirikisha na wengine katika ibada, ambao hawawezi kuondoa shari wala kuleta kheri!