Wale wanao ipinga Haki wala hawaifuati, na wanaendelea na uwovu wao mpaka wakafa nao ni wapinzani tu, basi yeyote miongoni mwao hawezi kujitolea fidia ya kujiepusha na adhabu ya Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taa'la, hata ikawa anacho kitoa kuwa fidia ni dhahabu ya kujaza dunia nzima kama angeweza. Na adhabu yao ina uchungu mkali.