Aidha wao husema: Msiwakubalie ila aliye fuata dini yenu, asije yeyote kati yao akadai kuwa nao wamepewa kama mlio pewa nyinyi, au akachukulia hoja mbele ya Mola wenu Mlezi kwa kuwakubalia kwenu. Ewe Nabii! Waambie: Hakika uwongofu wote unateremka kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye anaye mmiminia na kumteua amtakaye. Na ewe Nabii! Waambie: Hakika fadhila ziko kwa Mwenyezi Mungu humpa amtakaye katika waja wake, na Yeye ni Mkunjufu wa fadhila, Mjuzi wa anaye stahiki hayo na anaye teremkiwa na hayo.