Enyi Watu wa Kitabu! Kwa nini mkachukua Haki waliyo kuja nayo Manabii, na ikateremshiwa Vitabu, mkaichanganya na mambo ya udanganyifu ya kubuni na mkaleta tafsiri potovu, na msieneze Haki safi iliyo wazi isiyo kuwa na mchanganyiko? Na nyinyi mwajua vyema kuwa adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa kitendo kama hichi ni kubwa.