Mwenyezi Mungu amebainisha wazi katika maumbaji yake dalili na Ishara ambazo hawezi kuzipinga mwenye akili, ya kwamba Yeye ni Mmoja, wala hana mshirika wake, na kwamba Yeye ndiye Mwenye kusimamia mambo ya viumbe vyote kwa uadilifu. Na kwa haya pia wamekiri Malaika walio t'ahirika, na wameyajua watu wa ilimu kwa yakini, na kwamba Yeye ilio tukuka shani yake ni Mpweke katika Ungu, wala hana wa kumshinda katika jambo, na hikima yake imeenea kila kitu.