Hao wachamngu ndio wale wanao toa mali yao kwa kumridhi Mwenyezi Mungu wanapo kuwa na neema na wasaa, na pia wanapo kuwa na shida na dhiki na uzito, na wanazuia ghadhabu zao wanapo kasirishwa wasiwaadhibu wale wanao wakosa, bali wanawasamehe walio watendea mabaya. Hao kwa haya huhisabiwa kuwa ndio watenda mema. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu huwalipa mema hao watenda mema na huwa radhi nao.