Na lau kuwa Mwenyezi Mungu hakukufanyieni fadhila na akakurehemuni, na kuwa Yeye ni Mwingi wa kukubali toba za waja wake, na Mwenye hikima katika vitendo vyake vyote, asingeli kufanyieni sharia za hukumu hizi, na angeli fanya haraka kukuadhibuni duniani kwa maasia.