Maneno yao hayakumuathiri hata chembe. Akawajibu kwa kusema: Mimi sikukushitakieni, wala sikukutakeni mnipunguzie machungu yangu! Mimi sina ila Mwenyezi Mungu tu wa kumnyenyekea na kumshitakia dhiki zangu nzito na nyepesi. Wala siwezi kumficha hayo wala lolote nisilo liweza, kwani mimi natambua wema wake wa kutenda na ukunjufu wa rehema yake, jambo ambalo nyinyi hamlijui!