Wala haikufalia kwa Yusuf kuvunja mpango alio mkubalia Mwenyezi Mungu, na kumwachia nduguye atoke mkononi mwake. Kwa hivyo maombi yao hayakumlainisha kitu. Akawajibu jawabu mkato, kwa kuwaambia: Mimi najilinda kwa Mwenyezi Mungu isije nafsi yangu ikadhulumu kwa kumzuia yeyote yule isipo kuwa yule yule tuliye mkuta nayo mali yetu. Tukimchukua mwenginewe kwa kumuadhibu tutakuwa katika hao walio vuka mipaka kwa kumshika asiye na makosa kwa madhambi ya mwovu.