Wakasema: Ewe Swaleh! Hakika wewe ulikuwa kwetu mtu wa kutarajiwa mema, na kupendwa, na kutukuzwa katika nyoyo zetu, kabla ya haya unayo tuitia! Hivyo unatutaka tuache ibada waliyo kuwa wakiabudu baba zetu na tuliyo izoea sisi na wao? Hakika sisi tuna shaka na huo wito wako wa kumuabudu Mwenyezi Mungu Mmoja. Haya ni mambo ya kukutilia shaka na dhana mbovu wewe na huo wito wako!