Mnyenyekeeni Mwenyezi Mungu na huku mnamwomba akusameheni dhambi zenu. Kisha rejeeni kwake kwa kumuabudu kwa ikhlasi na vitendo vyema, ili apate kukustarehesheni starehe nzuri duniani mpaka utakapo kufikieni muda wenu uliyo kadiriwa, na apewe Akhera kila mwenye vitendo vyema malipo ya kazi yake na fadhila yake. Na pindi mkiyaacha haya ninayo kuitieni kwayo itakuwa mtajiletea adhabu. Na mimi nakukhofieni adhabu hii katika Siku Kubwa watakapo fufuliwa watu wote, na kutokea vitisho vikubwa kabisa!