ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

Al-An'am

external-link copy
1 : 6

ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَجَعَلَ ٱلظُّلُمَٰتِ وَٱلنُّورَۖ ثُمَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِرَبِّهِمۡ يَعۡدِلُونَ

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mwenye sifa ambazo zote ni sifa za ukamilifu, Mwenye neema za nje na za ndani, za kidini na za kidunia, Ambaye Aliumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, Aliumba giza na mwangaza kwa kupishana usiku na mchana. Katika hili pana ishara ya utukufu wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kuwa Yeye Peke Yake Anastahiki kuabudiwa. Haifai kwa yoyote kumshirikisha mwengine na Yeye. Na pamoja na uwazi huu, makafiri wanamsawazisha mwingine na Mwenyezi Mungu na wanamshirikisha na Yeye. info
التفاسير:

external-link copy
2 : 6

هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَكُم مِّن طِينٖ ثُمَّ قَضَىٰٓ أَجَلٗاۖ وَأَجَلٞ مُّسَمًّى عِندَهُۥۖ ثُمَّ أَنتُمۡ تَمۡتَرُونَ

Yeye Ndiye Ambaye Alimuumba baba yenu Ādam kutokana na udongo na nyinyi mnatokana na kizazi chake, kisha Akaandika muda wa kusalia kwenu katika uhai huu wa kilimwengu, na Akaandika muda mwingine maalumu hakuna aujuwao isipokuwa Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, nayo ni Siku ya Kiyama. Kisha nyinyi baada ya haya mnashuku juu ya uwezo wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wa kufufua baada ya kufa. info
التفاسير:

external-link copy
3 : 6

وَهُوَ ٱللَّهُ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَفِي ٱلۡأَرۡضِ يَعۡلَمُ سِرَّكُمۡ وَجَهۡرَكُمۡ وَيَعۡلَمُ مَا تَكۡسِبُونَ

Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakata na kila sifa ya upungufu, Ndiye Mola Mwenye kuabudiwa kwa haki mbinguni na ardhini. Na miongoni mwa dalili za uungu wake ni kwamba Yeye Anayajua yote mnayoyaficha, enyi watu, na mnayoyadhihirisha na Anayajua matendo yenu yote, mazuri na mabaya. Na kwa ajili hii, Yeye Peke Yake, Aliyetukuka na kuwa juu, Ndiye Mola Anayestahiki kuabudiwa. info
التفاسير:

external-link copy
4 : 6

وَمَا تَأۡتِيهِم مِّنۡ ءَايَةٖ مِّنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِمۡ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ

Makafiri hawa Ambao wanamshirikisha mwingine na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wamejiwa na hoja zilizo wazi na dalili dhahiri juu upweke wa Mwenyezi Mungu, Aiyetukuka na kuwa juu, na ukweli wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, juu ya utume wake na yale aliyokuja nayo. Lakini punde tu yalipowajia waliyaepuka na kukataa kuyakubali na wasiyaamini. info
التفاسير:

external-link copy
5 : 6

فَقَدۡ كَذَّبُواْ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ فَسَوۡفَ يَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Makafiri hawa waliikataa haki ambayo alikuja nayo Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na wakawafanyia shere walinganizi wake kwa sababu ya ujinga walionao kuhusu Mwenyezi Mungu na kughurika kwao na muhula Aliowapa. Basi watakuja kuyaona yale waliyoyafanyia shere kuwa ni haki na ni kweli. Na Mwenyezi Mungu Atawabainishia wakanushaji urongo wao na uzushi wao na awalipe kwa hayo. info
التفاسير:

external-link copy
6 : 6

أَلَمۡ يَرَوۡاْ كَمۡ أَهۡلَكۡنَا مِن قَبۡلِهِم مِّن قَرۡنٖ مَّكَّنَّٰهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مَا لَمۡ نُمَكِّن لَّكُمۡ وَأَرۡسَلۡنَا ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡهِم مِّدۡرَارٗا وَجَعَلۡنَا ٱلۡأَنۡهَٰرَ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهِمۡ فَأَهۡلَكۡنَٰهُم بِذُنُوبِهِمۡ وَأَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قَرۡنًا ءَاخَرِينَ

Kwani hawayajui, hawa wanaoukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kustahiki Kwake, Peke Yake, kuabudiwa na wanaomkanusha Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,, yale yaliyowashukia watu waliokanusha kabla yao ya maangamivu na uharibifu? Hao tuliwapa utulivu kwenye ardhi kwa namna ambayo hatukuwapa nyinyi, enyi makafiri, utulivu kama huo na tuliwaneemesha kwa kuwateremshia mivua na kupita mito chini ya makao yao kwa njia ya kuwanyoshea na kuwapa muhula, wakazikanusha neema za Mwenyezi Mungu na wakawakanusha Mitume. Hapo tuliwaangamiza kwa sababu ya madhambi yao na tukawaumba baada yao watu wengine walioshika nafasi zao katika kuiamirisha ardhi. info
التفاسير:

external-link copy
7 : 6

وَلَوۡ نَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ كِتَٰبٗا فِي قِرۡطَاسٖ فَلَمَسُوهُ بِأَيۡدِيهِمۡ لَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٞ

Na lau tulikuteremshia kitabu kutoka mbinguni, katika kurasa, wakazigusa washirikina hawa kwa mikono yao, wanagalisema, «Uliokuja nao ni uchawi ulio wazi uliobainika». info
التفاسير:

external-link copy
8 : 6

وَقَالُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ مَلَكٞۖ وَلَوۡ أَنزَلۡنَا مَلَكٗا لَّقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ ثُمَّ لَا يُنظَرُونَ

Na walisema washirikina hawa, «Si Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Amteremshie Muhammad Malaika kutoka mbinguni ili amsadiki kwa yale aliyokuja nayo Ya utume.» Na lau tulimteremsha Malaika kutoka mbinguni kwa kujibu ombi lao, uamuzi wa kuwaangamiza ungalipitishwa, na wasingepewa muhula wa kutubia, kwani imetangulia kwenye ujuzi wa Mwenyezi Mungu kuwa wao hawataamini. info
التفاسير: