ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
28 : 54

وَنَبِّئۡهُمۡ أَنَّ ٱلۡمَآءَ قِسۡمَةُۢ بَيۡنَهُمۡۖ كُلُّ شِرۡبٖ مُّحۡتَضَرٞ

Na uwape habari kwamba maji yamegawanywa baina ya watu wako na ngamia: ngamia ana siku yake na nyinyi mna siku yenu, kila siku ya kunywa atakuja yule ambaye ni siku yake aliyogawanyiwa, na atakatazwa yule ambaye si siku yake aliyogawanyiwa. info
التفاسير:

external-link copy
29 : 54

فَنَادَوۡاْ صَاحِبَهُمۡ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ

Wakamuita mwenzao wakimshawishi amchinje, basi akamshika yule ngamia kwa mkono wake na akamchinja, na mimi nikawatesa, info
التفاسير:

external-link copy
30 : 54

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

basi ilikuwa vipi nilivyowaadhibu kwa ukafiri wao na nilivyowaonya waliowaasi Mitume wangu? Hakika hiyo ilikuwa adhabu kubwa yenye uchungu. info
التفاسير:

external-link copy
31 : 54

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَكَانُواْ كَهَشِيمِ ٱلۡمُحۡتَظِرِ

Sisi tuliwateremshia Jibrili, akawapigia ukulele mmoja, wakatoeka hadi wa mwisho wao, wakawa ni kama nyasi zilizokauka zilizo nyepesi kuvunjika, zinazofanyiwa boma la ngamia na mifugo. info
التفاسير:

external-link copy
32 : 54

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na kwa hakika tumeyasahilisha matamko ya Qur’ani, ili isomwe na ihifadhiwe, na tumeyasahilisha maana yake, ili ifahamike na izingatiwe kwa anayetaka kuwaidhika na kuzingatia. Basi je kuna yoyote mwenye kuwaidhika nayo? info
التفاسير:

external-link copy
33 : 54

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطِۭ بِٱلنُّذُرِ

Walizikanusha watu wa Lūṭ aya za Mwenyezi Mungu walioonywa nazo. info
التفاسير:

external-link copy
34 : 54

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٖۖ نَّجَّيۡنَٰهُم بِسَحَرٖ

Sisi tuliwateremshia upepo mkali unaowarushia mawe, isipokuwa watu wa Lūṭ wa nyumbani, kwani wao tuliwaokoa na adhabu kipindi cha mwisho wa usiku, info
التفاسير:

external-link copy
35 : 54

نِّعۡمَةٗ مِّنۡ عِندِنَاۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي مَن شَكَرَ

ikiwa ni neema itokayo kwetu juu yao. Kama tulivyompa malipo mema Lūṭ na watu wake wa nyumbani, tukawapa neema na tukawaokoa na adhabu yetu ndivyo tunavyowalipa mema waliotuamini na kutushukuru. info
التفاسير:

external-link copy
36 : 54

وَلَقَدۡ أَنذَرَهُم بَطۡشَتَنَا فَتَمَارَوۡاْ بِٱلنُّذُرِ

Kwa hakika Lūṭ aliwaonya watu wake mateso ya Mwenyezi Mungu na adhabu Yake, wasimsikilize, bali walilifanyia shaka hilo na wakamkanusha. info
التفاسير:

external-link copy
37 : 54

وَلَقَدۡ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيۡفِهِۦ فَطَمَسۡنَآ أَعۡيُنَهُمۡ فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

Na kwa hakika walitaka kwake kufanya uchafu na wageni wake ambao ni Malaika, tukayafuta macho yao wasione chochote na wakaambiwa, «Onjeni adhabu yangu na onyo langu alilowaonya nalo Lūṭ, amani imshukie.» info
التفاسير:

external-link copy
38 : 54

وَلَقَدۡ صَبَّحَهُم بُكۡرَةً عَذَابٞ مُّسۡتَقِرّٞ

Na iliwajia kipindi cha asubuhi adhabu ya kuendelea, imejikita kwao mpaka iwafikishe kwenye adhabu ya Akhera. Adhabu yenyewe ni kuvurumizwa mawe na kuipindua miji yao kwa namna ambayo kulikokuwa juu kukawa chini, info
التفاسير:

external-link copy
39 : 54

فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

na wakaambiwa, «Onjeni adhabu yangu niliyowateremshia nyinyi kwa sababu ya ukafiri wenu na ukanushaji wenu onyo langu alilowaonya nalo Lūṭ, amani imshukie. info
التفاسير:

external-link copy
40 : 54

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na kwa hakika tumeyasahilisha matamko ya Qur’ani, ili isomwe na ihifadhiwe, na tumeyasahilisha maana yake, ili ifahamike na izingatiwe kwa anayetaka kuwaidhika na kuzingatia. Basi je kuna mwenye kuwaidhika nayo? info
التفاسير:

external-link copy
41 : 54

وَلَقَدۡ جَآءَ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ ٱلنُّذُرُ

Kwa hakika lilimjia Fir'awn na watu wake onyo letu la kuwatesa kwa ukafiri wao. info
التفاسير:

external-link copy
42 : 54

كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذۡنَٰهُمۡ أَخۡذَ عَزِيزٖ مُّقۡتَدِرٍ

Walizikanusha dalili zetu zote zenye kutolea ushahidi upweke wetu na unabii wa Manabii wetu, tukawatesa kwa adhabu mateso ya Mshindi Asiyeshindwa, Mweza wa Analolitaka. info
التفاسير:

external-link copy
43 : 54

أَكُفَّارُكُمۡ خَيۡرٞ مِّنۡ أُوْلَٰٓئِكُمۡ أَمۡ لَكُم بَرَآءَةٞ فِي ٱلزُّبُرِ

Je makafiri wenu, enyi mkusanyiko wa Makureshi, ni bora kuliko wale waliotangulia kutajwa miongoni mwa wale walioangamia kwa sababu ya kukanusha kwao? Au nyinyi mmeepushwa na mateso ya Mwenyezi Mungu kwa yaliyomo kwenye Vitabu vilivyoteremshwa kwa Mitume kwa kuwa mtasalimika na mateso? info
التفاسير:

external-link copy
44 : 54

أَمۡ يَقُولُونَ نَحۡنُ جَمِيعٞ مُّنتَصِرٞ

Au kwani wanasema makafiri wa Makkah, «Sisi ndio wenye ushupavu na busara, na jambo letu ni la pamoja. Sisi ni watu wa ushindi, na hatatushinda anayetutaka kwa ubaya.?» info
التفاسير:

external-link copy
45 : 54

سَيُهۡزَمُ ٱلۡجَمۡعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ

Utashindwa mkusanyiko wa makafiri wa Makkah mbele ya Waislamu na watakimbia. Na hili lilitokea siku ya vita vya Badr. info
التفاسير:

external-link copy
46 : 54

بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوۡعِدُهُمۡ وَٱلسَّاعَةُ أَدۡهَىٰ وَأَمَرُّ

Na wakati wa Kiyama ambao ndio agizo la wao kulipwa wanachostahiki, na Wakati wa Kiyama ni mkubwa na mgumu zaidi kuliko adhabu iliyowafika siku ya Badr. info
التفاسير:

external-link copy
47 : 54

إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٖ

Hakika wahalifu wa ukafiri wako katika hali ya kuduwaa kutoijua haki na wako kwenye usumbufu na adhabu. info
التفاسير:

external-link copy
48 : 54

يَوۡمَ يُسۡحَبُونَ فِي ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمۡ ذُوقُواْ مَسَّ سَقَرَ

Siku watakapokokotwa ndani ya Moto kwa nyuso zao na waambiwe, «Onjeni ukali wa adhabu ya moto wa Jahanamu.» info
التفاسير:

external-link copy
49 : 54

إِنَّا كُلَّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَٰهُ بِقَدَرٖ

Hakika sisi kila kitu tumekiumba kwa kipimo tulichokikadiri na kukipitisha, na ilitangulia elimu yetu ya kukijua kitu hiko na kukiandika kwenye Ubao Uliohifadhiwa. info
التفاسير: