ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
63 : 33

يَسۡـَٔلُكَ ٱلنَّاسُ عَنِ ٱلسَّاعَةِۖ قُلۡ إِنَّمَا عِلۡمُهَا عِندَ ٱللَّهِۚ وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّ ٱلسَّاعَةَ تَكُونُ قَرِيبًا

Wanakuuliza watu , ewe Mtume, kuhusu kipindi cha Kiyama kwa njia ya kukiona ni kitu ambacho ni mbali kutokea na kwa njia ya kukikanusha. Waambie, «Hakika ya mambo ni kwamba Ujuzi wa kipindi cha Kiyama uko kwa Mwenyezi Mungu.» Na ni lipi linalokujuza wewe, ewe Mtume kwamba huenda Kiyama kikawa karibu? info
التفاسير:

external-link copy
64 : 33

إِنَّ ٱللَّهَ لَعَنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ وَأَعَدَّ لَهُمۡ سَعِيرًا

Mwenyezi Mungu Amewafukuza makafiri kwenye rehema Yake duniani na Akhera na Amewaandalia huko Akhera Moto wenye kuwashwa ulio na joto kali, info
التفاسير:

external-link copy
65 : 33

خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ لَّا يَجِدُونَ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرٗا

hali ya kukaa milele humo. Hawatapata mtegemewa wa kuwasaidia na kuwatetea, wala mwenye himaya wa kuwahami, Akawatoa Motoni. info
التفاسير:

external-link copy
66 : 33

يَوۡمَ تُقَلَّبُ وُجُوهُهُمۡ فِي ٱلنَّارِ يَقُولُونَ يَٰلَيۡتَنَآ أَطَعۡنَا ٱللَّهَ وَأَطَعۡنَا ٱلرَّسُولَا۠

Siku zitakapogeuzwa nyuso za makafiri Motoni, huku wakisema kwa kujuta na kuduwaa, «Tunatamani lau tungalimtii Mwenyezi Mungu na tungalimtii Mtume Wake duniani tukawa watu wa Peponi.» info
التفاسير:

external-link copy
67 : 33

وَقَالُواْ رَبَّنَآ إِنَّآ أَطَعۡنَا سَادَتَنَا وَكُبَرَآءَنَا فَأَضَلُّونَا ٱلسَّبِيلَا۠

Na watasema makafiri Siku ya Kiyama, «Mola wetu! Kwa kweli sisi tumewatii viongozi wetu katika upotevu na wakubwa wetu katika ushirikina wakatuepusha na njia ya uongofu na Imani. info
التفاسير:

external-link copy
68 : 33

رَبَّنَآ ءَاتِهِمۡ ضِعۡفَيۡنِ مِنَ ٱلۡعَذَابِ وَٱلۡعَنۡهُمۡ لَعۡنٗا كَبِيرٗا

Mola wetu! Waadhibu Motoni mara mbili zaidi ya adhabu unayotuadhibu kwayo, na uwafukuze kutoka kwenye rehema mafukuzo makali.» Katika hii pana dalili ya kwamba kumtii asiyekuwa Mwenyezi Mungu katika kuenda kinyume na amri Yake na amri ya Mtume Wake, kunapasisha kupata hasira za Mwenyezi Mungu na mateso Yake, na kwamba mfuasi na mfuatwa watashirikiana kwenye adhabu. Basi ajihadhari na hilo Muislamu. info
التفاسير:

external-link copy
69 : 33

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ ءَاذَوۡاْ مُوسَىٰ فَبَرَّأَهُ ٱللَّهُ مِمَّا قَالُواْۚ وَكَانَ عِندَ ٱللَّهِ وَجِيهٗا

Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo, msimkere Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa maneno wala kwa vitendo, wala msiwe mfano wa wale waliomkera Nabii wa Mwenyezi Mungu Mūsā, Mwenyezi Mungu Akamuepusha na kile walichokisema cha urongo na uzushi, na yeye alikuwa kwa Mwenyezi Mungu ni mwenye cheo kikubwa na utukufu. info
التفاسير:

external-link copy
70 : 33

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَقُولُواْ قَوۡلٗا سَدِيدٗا

Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo, fanyeni matendo ya kumtii na mjiepushe na matendo ya kumuasi, ili msistahili kupata mateso hayo. Na semeni, katika hali zenu zote na mambo yenu yote, maneno ya kunyoka na yanayolingana na usawa, yasiyokuwa na urongo na ubatilifu. info
التفاسير:

external-link copy
71 : 33

يُصۡلِحۡ لَكُمۡ أَعۡمَٰلَكُمۡ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۗ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَقَدۡ فَازَ فَوۡزًا عَظِيمًا

Mkimuogopa Mwenyezi Mungu na mkasema maneno ya sawa, Mwenyezi Mungu Atawasamehe dhambi zenu, Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, katika kile alichokiamrisha na akakikataza, basi huyo amefaulu kupata utukufu mkubwa duniani na Akhera. info
التفاسير:

external-link copy
72 : 33

إِنَّا عَرَضۡنَا ٱلۡأَمَانَةَ عَلَى ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱلۡجِبَالِ فَأَبَيۡنَ أَن يَحۡمِلۡنَهَا وَأَشۡفَقۡنَ مِنۡهَا وَحَمَلَهَا ٱلۡإِنسَٰنُۖ إِنَّهُۥ كَانَ ظَلُومٗا جَهُولٗا

Sisi tuliiorodhesha amana- ambayo Mwenyezi Mungu Amewapatia waliokalifishwa na Sheria waitunze, nayo ni kufuata maamrisho na kujiepusha na makatazo- kwa mbingu, ardhi na majabali, vikakataa kuibeba na vikaogopa visiweze kusimama kuitekeleza, na akaibeba binadamu na akashikamana nayo pamoja na udhaifu Wake. Hakika yeye ni mwingi wa udhalimu na ujinga wa nafsi yake. info
التفاسير:

external-link copy
73 : 33

لِّيُعَذِّبَ ٱللَّهُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ وَٱلۡمُشۡرِكَٰتِ وَيَتُوبَ ٱللَّهُ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمَۢا

Ili mwisho wa binadamu kuibeba amana uwe ni Mwenyezi Mungu kuwaadhibu wanafiki wa kiume wanaodhihirisha Uislamu na kuficha ukafiri na wanafiki wa kike, na wanaume wanaomshirikisha katika ibada ya Mwenyezi Mungu asiyekuwa Yeye na wanawake washirikina, na ili Awakubalie toba Waumini wa kiume na Waumini wa kike kwa kuzificha dhambi zao na kuacha kuwaadhibu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha kwa wenye kutubia miongoni mwa waja Wake, ni Mwenye huruma kwao. info
التفاسير: