ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
21 : 32

وَلَنُذِيقَنَّهُم مِّنَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَدۡنَىٰ دُونَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَكۡبَرِ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na tutawaonjesha, tena tutawaonjesha, hawa waasi wenye kukanusha adhabu ndogo ya matatizo, shida na misiba ya duniani kabla ya adhabu kubwa zaidi Siku ya Kiyama, ambako wataadhibiwa ndani ya moto wa Jahanamu, huenda wao wakarejea na wakatubia dhambi zao kwa Mola wao. info
التفاسير:

external-link copy
22 : 32

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّن ذُكِّرَ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِۦ ثُمَّ أَعۡرَضَ عَنۡهَآۚ إِنَّا مِنَ ٱلۡمُجۡرِمِينَ مُنتَقِمُونَ

Hakuna hata mmoja aliye dhalimu zaidi wa nafsi yake kuliko yule aliyekumbushwa dalili za Mwenyezi Mungu kisha akazipa mgongo zote, asiwaidhike kwa mawaidha yake, bali akayafanyia kiburi. Hakika sisi ni wenye kuwatesa wale wahalifu waliozipa mgongo aya za Mwenyezi Mungu na hoja Zake na wasinufaike nazo. info
التفاسير:

external-link copy
23 : 32

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ فَلَا تَكُن فِي مِرۡيَةٖ مِّن لِّقَآئِهِۦۖ وَجَعَلۡنَٰهُ هُدٗى لِّبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ

Hakika tulimletea Mūsā Taurati kama tulivyokuletea wewe, ewe Mtume, Qur’ani. Basi usiwe na shaka ya kukutana na Mūsā usiku wa Isrā’ (safari ya kwenda Bayt al- Maqdis) na Mi’rāj (safari ya kwenda mbinguni), na tukaifanya Taurati ni uongofu kwa Wana wa Isrāīl, Unawalingania kwenye haki na kwenye njia iliyonyoka. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 32

وَجَعَلۡنَا مِنۡهُمۡ أَئِمَّةٗ يَهۡدُونَ بِأَمۡرِنَا لَمَّا صَبَرُواْۖ وَكَانُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يُوقِنُونَ

Na tuliwafanya, miongoni mwa Wana wa Isrāīl, ni waongozi na walinganizi kwenye wema, watu wanawafuata na wao wanawalingania kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumuabudu Peke Yake na kumtii. Na walipata daraja hii ya juu waliposubiri juu ya amri za Mwenyezi Mungu, kuyaacha makemeo Yake na kuwalingania na kuvumilia makero katika njia Yake, na walikuwa wanaziamini kikweli aya za mwenyezi Mungu na hoja Zake. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 32

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَفۡصِلُ بَيۡنَهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فِيمَا كَانُواْ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ

Hakika Mola wako, ewe Mtume, Atatoa uamuzi baina ya Waumini na makafiri miongoni mwa Wana wa Isrāīl na wasiokuwa wao Siku ya Kiyama kwa uadilifu katika yale waliotafautiana juu yake miongoni mwa mambo ya dini, na Atamlipa kila binadamu kwa matendo yake kwa kuwatia watu wa Peponi Peponi na watu wa Motoni Motoni. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 32

أَوَلَمۡ يَهۡدِ لَهُمۡ كَمۡ أَهۡلَكۡنَا مِن قَبۡلِهِم مِّنَ ٱلۡقُرُونِ يَمۡشُونَ فِي مَسَٰكِنِهِمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٍۚ أَفَلَا يَسۡمَعُونَ

Kwani haikuwabainikia hawa wenye kumkanusha Mtume ni mara ngapi tuliwaangamiza ummah waliotangulia kabla yao na huku wanatembea kwenye makazi yao, wakawa wanayaona waziwazi, kama vile watu wa Hūd, Ṣāliḥ na Lūṭ? Hakika katika hayo kuna alama na mawaidha ya kutolea ushahidi ukweli wa Mitume waliowajia na urongo wa ushirikina walionao. Basi kwani hawasikii, hawa wenye kuwakanusha Mitume, mawaidha ya Mwenyezi Mungu na dalili Zake wakapata kunufaika nayo? info
التفاسير:

external-link copy
27 : 32

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا نَسُوقُ ٱلۡمَآءَ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ ٱلۡجُرُزِ فَنُخۡرِجُ بِهِۦ زَرۡعٗا تَأۡكُلُ مِنۡهُ أَنۡعَٰمُهُمۡ وَأَنفُسُهُمۡۚ أَفَلَا يُبۡصِرُونَ

Kwani hawakuona wenye kukanusha kufufuliwa baada ya kufa kwamba sisi tunayapeleka maji kwenye ardhi kavu iliyo ngumu ambayo haina mimea, tukatoa kwa maji hayo mimea yenye rangi mbalimbali yenye kuliwa na wanyama wao na miili yao ikapata chakula cha kuwafanya wao waishi kwayo? Kwani hawazioni neema hizi kwa macho yao wakajua kwamba Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kuwahuisha wafu na kuwafufua kutoka makaburini mwao? info
التفاسير:

external-link copy
28 : 32

وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا ٱلۡفَتۡحُ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Hawa washirikina wanaifanyia haraka adhabu, wanasema, «Ni lini hukumu hii ya kutuadhibu, kama mnavyodai, ambayo itaamua baina yetu na nyinyi, iwapo nyinyi ni wakweli katika madai yenu?» info
التفاسير:

external-link copy
29 : 32

قُلۡ يَوۡمَ ٱلۡفَتۡحِ لَا يَنفَعُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِيمَٰنُهُمۡ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ

Waambie, ewe Mtume, «Siku ya hukumu ambayo mtateswa na mtashuhudia kifo, makafiri hakutawafaa kuamini kwao, wala hawatacheleweshwa ili watubie na warudie.» info
التفاسير:

external-link copy
30 : 32

فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ وَٱنتَظِرۡ إِنَّهُم مُّنتَظِرُونَ

Basi wape mgongo, ewe Mtume, hawa washirikina, na usiujali ukanushaji wao, na ungojee vile Mwenyezi Mungu Atawafanya. Hakika wao ni wenye kungojea na kutaraji mpatikane na ubaya. Basi Mwenyezi Mungu Atawapa hizaya na Atawadhalilisha na Akupe ushindi juu yao. Na Mwenyezi Mungu Ashalifanya hilo, sifa njema ni Zake na wema ni Wake. info
التفاسير: