ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
47 : 22

وَيَسۡتَعۡجِلُونَكَ بِٱلۡعَذَابِ وَلَن يُخۡلِفَ ٱللَّهُ وَعۡدَهُۥۚ وَإِنَّ يَوۡمًا عِندَ رَبِّكَ كَأَلۡفِ سَنَةٖ مِّمَّا تَعُدُّونَ

Na makafiri wa Kikureshi, kwaujinga wao, wanakuharakisha, ewe Mtme, uwaletee adhabu ambayo uliwaonya nayo baada ya kuwa wakakamavu juu ya ukafiri. Mwenyezi Mungu Hataenda kinyume na ahadi yake ya adhabu aliyowaonya nayo, haina budi kutuka. Na hapa duniani Aliwaharakishia hiyo, siku ya vita vya Badr. Na siku moja miongoni mwa siku mbele ya Mwenyezi Mungu ni kama miaka alfu moja mnazozihesbu katika miaka duniani. info
التفاسير:

external-link copy
48 : 22

وَكَأَيِّن مِّن قَرۡيَةٍ أَمۡلَيۡتُ لَهَا وَهِيَ ظَالِمَةٞ ثُمَّ أَخَذۡتُهَا وَإِلَيَّ ٱلۡمَصِيرُ

Kuna miji mingi ilikuwa kwenye udhalimu, kwa ukakamavu wa watu wake juu ya ukafiri, nikawapa muda , na sikuwaharakishia adhabu na kwa hivyo wakaghurika, kisha nikawachukuwa kwa kuwaadhibu katika hii dunia, na ni kwangu ndio marejeo yao baada ya kuangamia kwao nitawapa adhabu wanayostahili info
التفاسير:

external-link copy
49 : 22

قُلۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّمَآ أَنَا۠ لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Sema, ewe Mtume, «Enyi watu! Mimi si kuwa isipokuwa ni muonyaji kwenu mwenye kumfikishia Mwenyezi Mungu ujumbe Wake. info
التفاسير:

external-link copy
50 : 22

فَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَرِزۡقٞ كَرِيمٞ

Basi wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na imani hiyo ikajikita kwenye nyoyo zao na wakafanya matendo mema, watapata msamaha wa dhambi zao kutoka kwa Mola wao na sitara ya kufinika matendo ya uasi yaliyotokana na wao na riziki nzuri isiyokatika nayo ni Pepo. info
التفاسير:

external-link copy
51 : 22

وَٱلَّذِينَ سَعَوۡاْ فِيٓ ءَايَٰتِنَا مُعَٰجِزِينَ أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَحِيمِ

Na wale wenye kujitahidi kufanya vitimbi ili kuzitangua aya za Qur’ani kwa kuzikanusha hali ya kuwa ni watesi na washindani, basi hao ndio watu wa Moto wenye kuwaka, wataungia na watasalia humo milele.» info
التفاسير:

external-link copy
52 : 22

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ مِن رَّسُولٖ وَلَا نَبِيٍّ إِلَّآ إِذَا تَمَنَّىٰٓ أَلۡقَى ٱلشَّيۡطَٰنُ فِيٓ أُمۡنِيَّتِهِۦ فَيَنسَخُ ٱللَّهُ مَا يُلۡقِي ٱلشَّيۡطَٰنُ ثُمَّ يُحۡكِمُ ٱللَّهُ ءَايَٰتِهِۦۗ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٞ

Na hatukuwatumiliza kabla yako wewe, ewe Mtume, Mtume yoyote wala Nabii isipokuwa asomapo kitabu cha Mwenyezi mungu, Shetani anatia katika kisomo chake wasiwasi na tashwishi, ili kuwazuilia watu kufuata kile anachokisoma. Lakini Mwenyezi Mungu Anatangua vitimbi vya Shetanai, Anauondoa ushawishi wake na Anathibitisha aya Zake zilizo wazi. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyokuwa na yatakayokuwa, hakuna kinachofichika Kwake chochote, ni Mwingi wa hekima katika makadirio Yake na amri Zake. info
التفاسير:

external-link copy
53 : 22

لِّيَجۡعَلَ مَا يُلۡقِي ٱلشَّيۡطَٰنُ فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡقَاسِيَةِ قُلُوبُهُمۡۗ وَإِنَّ ٱلظَّٰلِمِينَ لَفِي شِقَاقِۭ بَعِيدٖ

Na hakikua kitendo hiki kutoka kwa Shetani isipokuwa Mwenyezi Mungu Akifanye ni mtihani kwa wale ambao ndani ya nyoyo zao muna shaka na unafiki na kwa wale washirikina washupavu wa nyoyo ambao haliathiri kwao kemeo lolote. Na kwa hakika, madhalimu miongoni mwa hawa na wale wako kwenye uadui mkubwa na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na upingaji haki ulio mbali na usawa. info
التفاسير:

external-link copy
54 : 22

وَلِيَعۡلَمَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكَ فَيُؤۡمِنُواْ بِهِۦ فَتُخۡبِتَ لَهُۥ قُلُوبُهُمۡۗ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَهَادِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Na ili wapate kujua wenye elimu ambao wanapambanua, kwa ujuzi wao, baina ya ukweli na urongo kwamba Qur’ani tukufu ndio haki iliyoteremka juu yako, ewe Mtume, kutoka kwa Mwenyezi Mungu, haina udanganyifu ndani yake na hakuna njia yoyote ya Shetani kuifikia, na kwa hiyo imani yao inaongezeka na nyoyo zao zinainyenyekea. Na hakika ya Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaongoa wale walioiamini na wakamuamini Mtume Wake kwenye njia ya haki iliyo wazi, nayo ni Uislamu, na Atawaokoa kwayo na upotevu. info
التفاسير:

external-link copy
55 : 22

وَلَا يَزَالُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي مِرۡيَةٖ مِّنۡهُ حَتَّىٰ تَأۡتِيَهُمُ ٱلسَّاعَةُ بَغۡتَةً أَوۡ يَأۡتِيَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَقِيمٍ

Na hawataacha makafiri wenye kukanusha kuendelea kuwa kwenye shaka juu ya Qur’ani uliokuja nayo mpaka Kiyama kiwajie kwa ghafula na hali wao wako juu ya ukanushaji wao, au iwajie wao adhabu ya Siku isiyokuwa na wema ndani yake, nayo ni Siku ya kiyama. info
التفاسير: