ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
19 : 14

أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۚ إِن يَشَأۡ يُذۡهِبۡكُمۡ وَيَأۡتِ بِخَلۡقٖ جَدِيدٖ

Je, hujui, ewe mwenye kwambiwa,- na makusudiwa ni watu kwa jumla- kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyepatisha mbingu na ardhi kwa namna thabiti yenye kuonyesha hekima Yake , na kwamba Yeye Hakuziumba kwa mchezo, bali ni kwa ajili ya kutolea ushahidi juu ya upweke Wake na ukamilifu wa uweza Wake, ili wamuabudu Peke Yake, na wasimshirikishe na kitu chochote? Basi Akitaka Atawaondoa na Awalete watu wasiokuwa nyinyi wanaomtii Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
20 : 14

وَمَا ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ بِعَزِيزٖ

Na kuwaangamiza nyinyi na kuwaleta watu wengine wasiokuwa nyinyi si jambo lisilowezekana kwa Mwenyezi Mungu, bali ni jambo lilio pesi. info
التفاسير:

external-link copy
21 : 14

وَبَرَزُواْ لِلَّهِ جَمِيعٗا فَقَالَ ٱلضُّعَفَٰٓؤُاْ لِلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُوٓاْ إِنَّا كُنَّا لَكُمۡ تَبَعٗا فَهَلۡ أَنتُم مُّغۡنُونَ عَنَّا مِنۡ عَذَابِ ٱللَّهِ مِن شَيۡءٖۚ قَالُواْ لَوۡ هَدَىٰنَا ٱللَّهُ لَهَدَيۡنَٰكُمۡۖ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَجَزِعۡنَآ أَمۡ صَبَرۡنَا مَا لَنَا مِن مَّحِيصٖ

Na watatoka viumbe kwenye makaburi yao na watajitokeza waziwazi Siku ya Kiyama kwa Mwenyezi Mungu Aliye Mmoja Mwenye kutendesha nguvu, ili Awahukumu baina yao. Hapo wafuasi watasema kuwaambia viongozi wao , «Sisi tulikuwa kwenu nyinyi ulimwenguni ni wafuasi, tukifuata amri zenu. Je, nyinyi ni wenye kututetea na kuizuia chochote miongoni mwa adhabu ya Mwenyezi Mungu kama mlivyokuwa mkituahidi? Viongozi watasema, «Lau Mwenyezi Mungu Alituongoza kwenye Imani tungaliwalekeza kwenye hiyo, lakini Yeye Hakutuafikia ndipo tukapotea na tukawapoteza. Ni sawa kwetu sisi na kwenu kuwa na babaiko au kuvumilia, kwani hatuna pa kukimbilia kuepukana na adhabu wala pa kupata uokozai. info
التفاسير:

external-link copy
22 : 14

وَقَالَ ٱلشَّيۡطَٰنُ لَمَّا قُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ إِنَّ ٱللَّهَ وَعَدَكُمۡ وَعۡدَ ٱلۡحَقِّ وَوَعَدتُّكُمۡ فَأَخۡلَفۡتُكُمۡۖ وَمَا كَانَ لِيَ عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنٍ إِلَّآ أَن دَعَوۡتُكُمۡ فَٱسۡتَجَبۡتُمۡ لِيۖ فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوٓاْ أَنفُسَكُمۖ مَّآ أَنَا۠ بِمُصۡرِخِكُمۡ وَمَآ أَنتُم بِمُصۡرِخِيَّ إِنِّي كَفَرۡتُ بِمَآ أَشۡرَكۡتُمُونِ مِن قَبۡلُۗ إِنَّ ٱلظَّٰلِمِينَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Shetani atasema baada ya Mwenyezi Mungu kuamua jambo Lake na kuwahesabu viumbe Vyake, na kuingia watu wa Peponi Peponi na watu wa Motoni Motoni, «Mwenyezi Mungu Aliwaahidi nyinyi ahadi ya kweli ya kufufuliwa na kulipwa, na mimi niliwaahidi ahadi ya urongo kwamba hakuna kufufuliwa wala kulipwa, nikakawaendea kinyume na ahadi yangu. Na mimi si kuwa na nguvu zozote za kuwalazimisha kunifuata, wala si kuwa na hoja. Isipokuwa mimi niliwaita kwenye ukafiri na upotevu mkanifuata. Basi msinilaumu, jilaumuni nyinyi wenyewe. Dhambi ni dhambi zenu wenyewe. Mimi si mwenye kuwaokoa na nyinyi si wenye kunokoa na adhabu ya Mwenyezi Mungu. Mimi nimejiepusha na jambo la nyinyi kunifanya mimi ni mshirika pamoja na Mwenyezi Mungu katika kutiiwa ulimwenguni. Hakika madhalimu, katika kuupa mgongo kwao ukweli na kuufuata urongo, watakua na adhabu kali iumizayo. info
التفاسير:

external-link copy
23 : 14

وَأُدۡخِلَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا بِإِذۡنِ رَبِّهِمۡۖ تَحِيَّتُهُمۡ فِيهَا سَلَٰمٌ

Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya matendo mema, watatiwa ndani ya mabustani ya Pepo ambayo chini ya miti yake na majumba yake ya fahari inapita mito. Hawatatoka humo milele, kwa idhini ya Mola wao na uweza Wake na nguvu Zake. Watasalimiwa humo kwa salamu itokayo kwa Mwenyezi Mungu, Malaika Zake na Waumini. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 14

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا كَلِمَةٗ طَيِّبَةٗ كَشَجَرَةٖ طَيِّبَةٍ أَصۡلُهَا ثَابِتٞ وَفَرۡعُهَا فِي ٱلسَّمَآءِ

Kwani huoni, ewe Mtume, namna gani Mwenyezi Mungu alivolipiga mfano neno la tawhīd «Lā ilahā illā Allāh» wa mti mkubwa, nao ni mtende, ambao shina lake limejikita imara ndani ya ardhi na kilele chake kiko juu kimeelekea mbiguni? info
التفاسير: