Na uingize mkono wako kwenye uwazi wa nguo yako utatoka mweupe, bila ya ila wala maradhi. Na jiambatishe mkono wako ubavuni mwako katika nguo ukiwa una khofu. Wala usishituke kwa kuona fimbo imekuwa nyoka, na kuona mkono wako umekuwa mweupe. Kwani miujiza hii miwili inatokana na Mwenyezi Mungu ya kumkabili nayo Firauni na kaumu yake watapo ukabili Ujumbe wako kwa kuukadhibisha na hali wametoka kwenye ut'iifu wa Mwenyezi Mungu.