क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस

पृष्ठ संख्या:close

external-link copy
84 : 3

قُلۡ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ عَلَيۡنَا وَمَآ أُنزِلَ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَٱلۡأَسۡبَاطِ وَمَآ أُوتِيَ مُوسَىٰ وَعِيسَىٰ وَٱلنَّبِيُّونَ مِن رَّبِّهِمۡ لَا نُفَرِّقُ بَيۡنَ أَحَدٖ مِّنۡهُمۡ وَنَحۡنُ لَهُۥ مُسۡلِمُونَ

Waambie, ewe Mtume, «Tumemuamini Mwenyezi mungu na tumetii. Hatuna Mola isipokuwa Yeye, na hatuna muabudiwa isipokuwa Yeye. Tumeuamini wahyi Aliouteremsha kwetu na ule Aliouteremsha kwa Ibrāhīm aliye rafiki halisi wa Mwenyezi Mungu, na wanawe wawili, Ismā'il na Is’ḥāq, na mwana wa mwanawe,Ya'qūb mwana wa Is’ḥāq, na Asbāṭ: nao ni Manabii waliokuwa katika makabila kumi na mbili wanaotokana na watoto wa Ya'qūb, na wahyi uliopewa Mūsā na ‘Īsā wa Taurati na Injili, na wahyi Aliouteremsha Mwenyezi Mungu kwa Manabii Wake. Tunayaamini hayo yote. Wala hatumbagui yoyote katika wao. Na sisi tunamfuata Mwenyezi Mungu Peke Yake kwa kumtii na kumuabudu, tunakiri Kwake kuwa Yeye Ndiye Mola, Ndiye Mungu na Ndiye wa kuabudiwa info
التفاسير:

external-link copy
85 : 3

وَمَن يَبۡتَغِ غَيۡرَ ٱلۡإِسۡلَٰمِ دِينٗا فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡهُ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

Na Mwenye kutafuta dini isiyokuwa dini ya Kiislamu, ambayo ni kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kumpwekesha na kumfuata kwa kumtii na kumdhalilikia, na kwa Mtume wake aliye Nabii wa mwisho Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa kumuamini na kumfuata na kumpenda kwa dhahiri na kwa siri, basi hiyo haitakubaliwa kwake, na yeye Akhera atakuwa ni miongoni mwa wenye kupata hasara ambao walizifanyia ubahili nafsi zao kwa kuzinyima mambo yenye kuzinufaisha. info
التفاسير:

external-link copy
86 : 3

كَيۡفَ يَهۡدِي ٱللَّهُ قَوۡمٗا كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ وَشَهِدُوٓاْ أَنَّ ٱلرَّسُولَ حَقّٞ وَجَآءَهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُۚ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ

Vipi Mwenyezi Mungu Atawaafikia, wamuamini Yeye na wamfuate, watu walioukanusha unabii wa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, baada ya kuuamini na kushuhudia kuwa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni mkweli na yale aliyokuja nayo ni ya kweli na zikawajia wao hoja zinazotoka kwa Mwenyezi Mungu na dalili za usahihi wake? Na Mwenyezi Mungu Hawaafikii kwenye haki na usawa watu madhalimu, nao ni wale waliopotoka kwenye haki wakafuata batili, wakachagua ukafiri badala ya Imani. info
التفاسير:

external-link copy
87 : 3

أُوْلَٰٓئِكَ جَزَآؤُهُمۡ أَنَّ عَلَيۡهِمۡ لَعۡنَةَ ٱللَّهِ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ

Madhalimu hao, malipo yao ni kuwa wao watashukiwa na laana ya Mwenyezi Mungu na Malaika na watu wote. Wao wamefukuzwa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
88 : 3

خَٰلِدِينَ فِيهَا لَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابُ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ

Ni wenye kukaa milele Motoni; hawataondolewa adhabu kidogo ili wapumzike wala hawatacheleweshewa kwa udhuru wowote watakaoutoa. info
التفاسير:

external-link copy
89 : 3

إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ وَأَصۡلَحُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ

Isipokuwa waliorudi kwa Mola wao kwa kutubia kidhati baada ya ukafiri wao na udhalimu wao na wakayatengeneza, kwa toba yao, waliyoyaharibu. Mwenyezi Mungu Ataikubali hiyo toba, kwani Yeye ni Mwingi wa kusamehe madhambi ya waja wake, ni Mwenye huruma kwao. info
التفاسير:

external-link copy
90 : 3

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ ثُمَّ ٱزۡدَادُواْ كُفۡرٗا لَّن تُقۡبَلَ تَوۡبَتُهُمۡ وَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلضَّآلُّونَ

Hakika wale waliokufuru baada ya kuwa wao wameamini na wakaendelea kwenye ukafiri mpaka kufa, haitakubaliwa toba kutoka kwao mauti yakiwasimamia. Na wao ndio waliopotea njia wakakosa kuifikia. info
التفاسير:

external-link copy
91 : 3

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَمَاتُواْ وَهُمۡ كُفَّارٞ فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡ أَحَدِهِم مِّلۡءُ ٱلۡأَرۡضِ ذَهَبٗا وَلَوِ ٱفۡتَدَىٰ بِهِۦٓۗ أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ وَمَا لَهُم مِّن نَّٰصِرِينَ

Hakika wale waliokanusha unabii wa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na wakafa juu ya kumkufuru Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, haitakubaliwa kutoka kwa mmoja wao, Siku ya Kiyama, dhahabu iliyojaa ardhi iwe ni fidia ya nafsi yake kutokana na adhabu ya Mwenyezi Mungu, lau atajikomboa nayo kikweli. Wao wana adhabu yenye kuumiza; na hawana yoyote wa kuwaokoa na adhabu ya Mwenyezi Mungu. info
التفاسير: