Na Mwenyezi Mungu peke yake ndiye anaye zituma pepo ziyatimue mawingu yaliyo rindika kwa mvuke wa maji. Tena tukayasukuma hayo mawingu mpaka kwenye nchi yenye ukame, tukaihuisha ardhi yake baada ya kuwa ilikuwa imekufa. Kama tunavyo itoa mimea katika ardhi, basi hali kadhaalika tutawatoa maiti makaburini Siku ya Kiyama. Rejea maoni ya ki-ilimu juu ya Aya 57 katika Surat Al Aa'raaf.