કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષામાં અનુવાદ - અલી મોહસીન અલ્ બર્વાની

પેજ નંબર:close

external-link copy
64 : 12

قَالَ هَلۡ ءَامَنُكُمۡ عَلَيۡهِ إِلَّا كَمَآ أَمِنتُكُمۡ عَلَىٰٓ أَخِيهِ مِن قَبۡلُ فَٱللَّهُ خَيۡرٌ حَٰفِظٗاۖ وَهُوَ أَرۡحَمُ ٱلرَّٰحِمِينَ

Je, nikuaminini kwa huyu ila kama nilivyo kuaminini kwa nduguye zamani? Lakini Mwenyezi Mungu ndiye Mbora wa kulinda, naye ndiye Mbora wa kurehemu kuliko wenye kurehemu wote. info

Yaa'qub yalimtibuka moyoni mwake yale ya zamani, akayaunganisha na haya mapya. Akawaambia wanawe: Nikikukubalieni itakuwa hali yangu ni ya ajabu; kwani nikikuaminini kwa huyu ndugu yenu haitakuwa ila mfano wa pale nilipo kuaminini kwa Yusuf. Mkamchukua kisha mkarudi mkisema: Kaliwa na mbwa mwitu! Lakini Mwenyezi Mungu ndiye anaye nitosheleza katika kumlinda mwanangu. Wala mimi simtegemei mtu ila Yeye, kwani Yeye ndiye Mlinzi aliye na nguvu kuliko wote, na rehema yake ni kunjufu mno, hatonipa tena machungu ya ndugu yake baada ya yale ya Yusuf.

التفاسير:

external-link copy
65 : 12

وَلَمَّا فَتَحُواْ مَتَٰعَهُمۡ وَجَدُواْ بِضَٰعَتَهُمۡ رُدَّتۡ إِلَيۡهِمۡۖ قَالُواْ يَٰٓأَبَانَا مَا نَبۡغِيۖ هَٰذِهِۦ بِضَٰعَتُنَا رُدَّتۡ إِلَيۡنَاۖ وَنَمِيرُ أَهۡلَنَا وَنَحۡفَظُ أَخَانَا وَنَزۡدَادُ كَيۡلَ بَعِيرٖۖ ذَٰلِكَ كَيۡلٞ يَسِيرٞ

Na walipo fungua mizigo yao wakakuta bidhaa zao wamerudishiwa. Wakasema: Ewe baba yetu! Tutake nini zaidi? Hizi bidhaa zetu tumerudishiwa. Wacha tuwaletee watu wetu chakula, na tutamlinda ndugu yetu, na tutaongeza shehena ya ngamia. Na hicho ni kipimo kidogo. info

Na wale nduguze Yusuf hawakujua kuwa Yusuf aliwatilia bidhaa zao katika mizigo yao. Walipo ifungua wakakuta mali yao, na wakaona hisani aliyo wafanyia Yusuf, wakaitumia hiyo kuzidi kumpoza moyo Yaa'qub, na kumkinaisha awakubalie kwa aliyo yataka Mheshimiwa. Wakazidi kumshikilia akubali, wakamkumbusha makhusiano yao yalio wafunga kwa baba mmoja. Wakasema: Ewe baba yetu! Unataka wema gani zaidi kuliko haya, na hayo yatayo kuwa? Haya mali yetu tumerudishiwa bila ya kuchukuliwa chochote. Basi natusafiri na ndugu yetu, na tuwaletee watu wetu mahitaji, nasi tutamchunga ndugu yetu, na tutaongeza mahitaji shehena ya ngamia kuwa ni haki ya ndugu yetu! Kwani yule Mheshimiwa kapanga kuwa kila mtu humpa shehena ya ngamia.

التفاسير:

external-link copy
66 : 12

قَالَ لَنۡ أُرۡسِلَهُۥ مَعَكُمۡ حَتَّىٰ تُؤۡتُونِ مَوۡثِقٗا مِّنَ ٱللَّهِ لَتَأۡتُنَّنِي بِهِۦٓ إِلَّآ أَن يُحَاطَ بِكُمۡۖ فَلَمَّآ ءَاتَوۡهُ مَوۡثِقَهُمۡ قَالَ ٱللَّهُ عَلَىٰ مَا نَقُولُ وَكِيلٞ

Akasema: Sitampeleka nanyi mpaka mnipe ahadi kwa Mwenyezi Mungu kwamba lazima mtamrejeza kwangu, ila ikiwa mmezungukwa. Basi walipo mpa ahadi yao alisema: Mwenyezi Mungu ndiye Mtegemewa kwa tuyasemayo. info

Waliweza wana wa Yaa'qub kumkinaisha baba yao, na maneno yao yakampata palipo. Akaacha kushikilia kumzuia mwanawe asende Misri na nduguze. Lakini moyo wake haukuwacha kuwa na haja ya kuzidi kutuzwa. Kwa hivyo aliwaambia: Sitomwacha ende nanyi ila baada ya kunipa dhamana ya nguvu. Niahidini kwa Mwenyezi Mungu kwamba mtanirudishia mtapo rudi. Na wala msiache kumrudisha ila mkiangamia nyinyi au ikawa adui amekuzungukeni akakushindeni. Wakamkubalia na wakampa ahadi aliyo itaka. Na hapo tena akamshuhudisha Mwenyezi Mungu ahadi yao na viapo vyao kwa kusema: Mwenyezi Mungu anayashuhudia na kuyaona yote haya yanayo pita baina yetu.

التفاسير:

external-link copy
67 : 12

وَقَالَ يَٰبَنِيَّ لَا تَدۡخُلُواْ مِنۢ بَابٖ وَٰحِدٖ وَٱدۡخُلُواْ مِنۡ أَبۡوَٰبٖ مُّتَفَرِّقَةٖۖ وَمَآ أُغۡنِي عَنكُم مِّنَ ٱللَّهِ مِن شَيۡءٍۖ إِنِ ٱلۡحُكۡمُ إِلَّا لِلَّهِۖ عَلَيۡهِ تَوَكَّلۡتُۖ وَعَلَيۡهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُتَوَكِّلُونَ

Na akasema: Enyi wanangu! Msiingie mlango mmoja, bali ingieni kwa milango mbali mbali. Wala mimi sikufaeni kitu mbele ya Mwenyezi Mungu. Hukumu haiko ila kwa Mwenyezi Mungu tu. Juu yake Yeye mimi nimetegemea, na juu yake Yeye wategemee wanao tegemea. info

Yaa'qub alitua kwa ahadi ya watoto wake. Kisha huruma ilimpelekea kuwausia kuwa watapo ingia Misri waingie kupita milango mbali mbali, ili watu wasiwapige kijicho, huenda wakadhurika. Akasema: Wala mimi sina uwezo wa kukulindeni na madhara. Kwani mwenye kuzuia madhara ni Mwenyezi Mungu tu, na hukumu ni yake Yeye pekee. Mimi nimemtegemea Yeye, na mambo yangu na yenu yote nimemwachia Yeye. Na juu yake Yeye peke yake wategemee wote wanao tegemeza mambo yao, kwa kumuamini Yeye.

التفاسير:

external-link copy
68 : 12

وَلَمَّا دَخَلُواْ مِنۡ حَيۡثُ أَمَرَهُمۡ أَبُوهُم مَّا كَانَ يُغۡنِي عَنۡهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِن شَيۡءٍ إِلَّا حَاجَةٗ فِي نَفۡسِ يَعۡقُوبَ قَضَىٰهَاۚ وَإِنَّهُۥ لَذُو عِلۡمٖ لِّمَا عَلَّمۡنَٰهُ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَعۡلَمُونَ

Na walipo ingia kama alivyo waamrisha baba yao, haikuwafaa kitu kwa Mwenyezi Mungu, isipo kuwa ni haja tu iliyo kuwa katika nafsi ya Yaa'qub aliitimiza. Na hakika yeye alikuwa na ilimu kwa sababu tulimfundisha; lakini watu wengi hawajui. info

Wale vijana wakapokea wasia wa baba yao, wakapitia milango mbali mbali. Wala hayo si kama ndiyo ya kuwazuilia madhara walio kwisha andikiwa na Mwenyezi Mungu! Na Yaa'qub akijua hayo, kwani yeye alikuwa na ilimu tuliyo mfundisha. Lakini wasia wake ulikuwa ni kwa haja aliyo kuwa nayo nafsini mwake tu, nayo ni huruma ya baba kwa wanawe ambayo ameidhihirisha katika huu wasia. Na hakika watu wengi hawana ujuzi kama alio kuwa nao Yaa'qub wakamwachia mambo yao Mwenyezi Mungu awalinde.

التفاسير:

external-link copy
69 : 12

وَلَمَّا دَخَلُواْ عَلَىٰ يُوسُفَ ءَاوَىٰٓ إِلَيۡهِ أَخَاهُۖ قَالَ إِنِّيٓ أَنَا۠ أَخُوكَ فَلَا تَبۡتَئِسۡ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Na walipo ingia kwa Yusuf alimchukua nduguye akasema: Mimi hakika ni nduguyo. Basi usihuzunike kwa waliyo kuwa wakiyafanya. info

Walipo ingia kwa Yusuf aliwapokea kwa hishima, na khasa yule nduguye kwa baba na mama ndio akamchukua na akampa siri kwa kumwambia: Usitie shaka mimi ni nduguyo Yusuf. Basi usihuzunike kwa waliyo kufanyia wewe na waliyo nifanyia mimi.

التفاسير: