કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષામાં અનુવાદ - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ

પેજ નંબર:close

external-link copy
104 : 5

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ وَإِلَى ٱلرَّسُولِ قَالُواْ حَسۡبُنَا مَا وَجَدۡنَا عَلَيۡهِ ءَابَآءَنَآۚ أَوَلَوۡ كَانَ ءَابَآؤُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ شَيۡـٔٗا وَلَا يَهۡتَدُونَ

Na hawa makafiri, wanaoharamisha yaliyohalalishwa na Mwenyezi Mungu, wanapoambiwa, «Njooni kwenye hukumu zilizoteremshwa na Mwenyezi Mungu na uwamuzi wa Mtume Wake, ili halali na haramu ziwafunukie, wao huwa wakisema, «Yanatutosha yale tuliyoyarithi kwa baba zetu ya maneno na vitendo.» Je wanayasema hayo ingawa baba zao walikuwa hawajui chochote: yaani, hawaielewi haki, hawaitambui wala hawaongoki kuifikia? Basi vipi watawafuata na hali ni hii? Kwa kweli, hakuna mwenye kuwafuata isipokua mjinga zaidi kuliko wao na mpotevu zaidi wa njia. info
التفاسير:

external-link copy
105 : 5

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ عَلَيۡكُمۡ أَنفُسَكُمۡۖ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا ٱهۡتَدَيۡتُمۡۚ إِلَى ٱللَّهِ مَرۡجِعُكُمۡ جَمِيعٗا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na mkafuata sheria Yake kivitendo, jilazimisheni nafsi zenu kujishughulisha kumtii Mwenyezi Mungu na kujiepusha na kumuasi na endeleeni daima kufanya hivyo, hata kama watu hawatakubaliana na nyinyi. Mkifanya hivyo, hautawadhuru nyinyi upotevu wa mwenye kupotea madhali nyinyi mnajilazimisha na njia ya usawa, mnaamrisha mema na mnakataza maovu. Kwa Mwenyezi Mungu ndiko marejeo yenu nyote kesho Akhera, huko atawapa habari ya matendo yenu na atawapa malipo yake. info
التفاسير:

external-link copy
106 : 5

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ شَهَٰدَةُ بَيۡنِكُمۡ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ حِينَ ٱلۡوَصِيَّةِ ٱثۡنَانِ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ أَوۡ ءَاخَرَانِ مِنۡ غَيۡرِكُمۡ إِنۡ أَنتُمۡ ضَرَبۡتُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَأَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةُ ٱلۡمَوۡتِۚ تَحۡبِسُونَهُمَا مِنۢ بَعۡدِ ٱلصَّلَوٰةِ فَيُقۡسِمَانِ بِٱللَّهِ إِنِ ٱرۡتَبۡتُمۡ لَا نَشۡتَرِي بِهِۦ ثَمَنٗا وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰ وَلَا نَكۡتُمُ شَهَٰدَةَ ٱللَّهِ إِنَّآ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡأٓثِمِينَ

Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na mkafuata sheria Yake kivitendo, mmoja wenu akiwa karibu na kufa, basi ni juu yake awashuhudishe wasia wake waaminifu wawili miongoni mwa Waislamu, au wawili wengine miongoni mwa wasiokuwa Waislamu ikibidi hivyo, na kusiwe na Waislamu. Hao mtawashuhudisha iwapo muko safarini kwenye ardhi na mkafikiwa na kifo. Na iwapo mtautilia shaka ushahidi wao, wasimamisheni baada ya Swala, yaani, swala ya Waislamu, hasa Swala ya Alasiri, waape kwa Mwenyezi Mungu kiapo cha dhati kwamba wao hawachukui kwa ushahidi wao thamani ya kilimwengu kama badala, wala hawamfanyii mapendeleo jamaa yao na wala hawafichi kwa kiapo chao ushahidi wa Mwenyezi Mungu uliyoko kwao na kwamba wao wakilifanya hilo, basi wao watakuwa ni miongoni mwa waliofanya hatia. info
التفاسير:

external-link copy
107 : 5

فَإِنۡ عُثِرَ عَلَىٰٓ أَنَّهُمَا ٱسۡتَحَقَّآ إِثۡمٗا فَـَٔاخَرَانِ يَقُومَانِ مَقَامَهُمَا مِنَ ٱلَّذِينَ ٱسۡتَحَقَّ عَلَيۡهِمُ ٱلۡأَوۡلَيَٰنِ فَيُقۡسِمَانِ بِٱللَّهِ لَشَهَٰدَتُنَآ أَحَقُّ مِن شَهَٰدَتِهِمَا وَمَا ٱعۡتَدَيۡنَآ إِنَّآ إِذٗا لَّمِنَ ٱلظَّٰلِمِينَ

Wakigundua wanaohusika na maiti kuwa wale mashahidi wawili wamefanya makosa ya hiana katika ushahidi au wasia, basi na wasimame mahali pao pa ushahidi watu wawili wenye ujamaa na aliyekufa waape kwa Mwenyezi Mungu: Ushahidi wetu wa kweli unastahiki zaidi kukubaliwa kuliko ushahidi wao wa urongo. Na sisi hatukukiuka haki katika kutoa ushahidi wetu. Na tukifanya dhuluma na kutoa ushahidi usio wa haki, basi sisi tutakuwa ni miongoni mwa madhalimu wenye kukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
108 : 5

ذَٰلِكَ أَدۡنَىٰٓ أَن يَأۡتُواْ بِٱلشَّهَٰدَةِ عَلَىٰ وَجۡهِهَآ أَوۡ يَخَافُوٓاْ أَن تُرَدَّ أَيۡمَٰنُۢ بَعۡدَ أَيۡمَٰنِهِمۡۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱسۡمَعُواْۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡفَٰسِقِينَ

Hukumu hiyo ya kuapa baada ya Swala na kutokubali ushahidi wa hao wawili, baada ya kuutilia shaka, ndiyo inayouleta karibu zaidi uwezekano wa wao kutoa ushahidi kama ulivyo kwa kuogopa adhabu ya Akhera au kwa kuchelea yamini lao la urongo lisikataliwe na wale wenye haki baada ya kuapa kwao na asije akafedheheka yule mrongo ambaye yamini lake lilikakataliwa hapa ulimwenguni baada ya kufunuka uhaini wake. Na muogopeni Mwenyezi Mungu, enyi watu, na mumtunze msije mukaapa kiapo cha urongo na msije mkanyakuwa kwa mayamini yenu mali ya haramu. Na msikie mnayowaidhiwa nayo. Na Mwenyezi Mungu Hawaongozi watu wenye nyendo mbaya waliotoka nje ya utiifu Wake. info
التفاسير: