કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષામાં અનુવાદ - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ

પેજ નંબર:close

external-link copy
109 : 3

وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ

Na ni Vyake, Yeye Mwenyezi Mungu Peke Yake, vyote vilivyo mbinguni na vilivyo ardhini, ni milki Yake Pekee kwa kuviumba na kuvisimamia. Na marejeo ya viumbe wote ni Kwake Yeye Peke Yake, na Atamlipa kila mmoja kwa kadiri anayostahiki. info
التفاسير:

external-link copy
110 : 3

كُنتُمۡ خَيۡرَ أُمَّةٍ أُخۡرِجَتۡ لِلنَّاسِ تَأۡمُرُونَ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَتَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَتُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِۗ وَلَوۡ ءَامَنَ أَهۡلُ ٱلۡكِتَٰبِ لَكَانَ خَيۡرٗا لَّهُمۚ مِّنۡهُمُ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَأَكۡثَرُهُمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ

Nyinyi, enyi uma wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni bora wa ummah na ni watu wenye manufaa zaidi kwa watu, mnaamrisha mema, nayo ni yale yanayofahamika uzuri wake kisheria na kiakili, na mnakataza maovu , nayo ni yale yanayoeleweka ubaya wake kisheria na kiakili, na mnamuamini Mwenyezi Mungu kikweli-kweli imani inayotiliwa nguvu na vitendo. Na lau kama Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu wangalimuamini Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na yale aliyowajia nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu kama mlivyoamini nyinyi, lingekuwa hilo ni bora kwao dunianina Akhera. Katiika hao wako Waumini waukubalio ujumbe wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wanaoufuata kivitendo ujumbe huo, nao ni wachache. Na wengi wao ni watokaji nje ya dini ya Mwenyezi Mungu na twaa Yake. info
التفاسير:

external-link copy
111 : 3

لَن يَضُرُّوكُمۡ إِلَّآ أَذٗىۖ وَإِن يُقَٰتِلُوكُمۡ يُوَلُّوكُمُ ٱلۡأَدۡبَارَ ثُمَّ لَا يُنصَرُونَ

Hawatawadhuru nyinyi hawa watu waovu, miongoni mwa watu waliopewa Vitabu, isipokuwa kile kitakachoyaudhi masikizi yenu cha matamshi ya ushirikina na ukafiri na mengineyo. Na wakiwapiga vita, watashindwa na watakimbia hali ya kuwapa mgongo, kisha hawatapata ushindi juu yenu kwa hali yoyote. info
التفاسير:

external-link copy
112 : 3

ضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلذِّلَّةُ أَيۡنَ مَا ثُقِفُوٓاْ إِلَّا بِحَبۡلٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَحَبۡلٖ مِّنَ ٱلنَّاسِ وَبَآءُو بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَسۡكَنَةُۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ

Amejaalia Mwenyezi Mungu utwevu na unyonge kuwa ni jambo lenye kuambatana nao Mayahudi na wala haliwaepuki. Kwa hivyo, wao daima ni madhalili wenye kudharauliwa popote waliopo, isipokuwa watakapokuwa na mafungamano na Mwenyezi Mungu na makubaliano na watu ambayo kwayo watajiwekea usalama wa nafsi zao na mali zao. Hayo ndiyo mapatano ya kujidhamini kwao na kujilazimisha kwao kufuata hukumu za Uislamu. Na wamerudi nyuma wakiwa wamepata hasira za Mwenyezi Mungu zilizowastahili. Na wamepigwa na unyonge na umasikini. Kwa hivyo, humuoni Myahudi isipokuwa utamkuta ameshukiwa na hofu na babaiko kwa kuwaogopa Waumini. Hilo ndilo Alilowajaalia Mwenyezi Mungu kwa sababu ya kumkufuru kwao Mwenyezi Mungu, kukeuka kwao mipaka Yake na kuwaua kwao Manabii, kwa udhalimu na uonevu. Na hakuna lolote lililowafanya wao wawe majasiri wa kuyatenda haya isipokuwa ni kule kufanya kwao maasia na kukiuka kwao mipaka ya Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
113 : 3

۞ لَيۡسُواْ سَوَآءٗۗ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ أُمَّةٞ قَآئِمَةٞ يَتۡلُونَ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ ءَانَآءَ ٱلَّيۡلِ وَهُمۡ يَسۡجُدُونَ

Waliopewa Vitabu hawako sawa: kati yao liko kundi lifuatalo njia iliyolingana sawa juu ya amri ya Mwenyezi Mungu, lenye kumuamini Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na ambalo watu wake wanasimama usiku wakizisoma aya za Qur’ani tukufu na wakielekea kwa Mwenyezi Mungu kwa kumuomba katika Swala zao. info
التفاسير:

external-link copy
114 : 3

يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَيَأۡمُرُونَ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَيُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِۖ وَأُوْلَٰٓئِكَ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Wanamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, wanaamrisha mambo ya kheri yote na wanakataza aina zote za shari na wanakimbilia kufanya mema. Hao ni miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu wema. info
التفاسير:

external-link copy
115 : 3

وَمَا يَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَلَن يُكۡفَرُوهُۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُتَّقِينَ

Na kitendo chochote, kichache au kingi, kati ya vitendo vyema yatakayofanywa na kikundi hiki kilichoamini, hakitapotea mbele ya Mwenyezi Mungu. Bali watashukuriwa na watapewa malipo yake. Mwenyezi Mungu Anawajua zaidi wacha-Mungu ambao wametenda mema na wakajitenga na yaliyoharamishwa kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kutaka thawabu Zake. info
التفاسير: