Na Wewe kwa ulivyo umba na ukawekea sababu na nyendo, unauingiza usiku katika mchana kwa unavyo zidi mchana urefu wake, na unauingiza mchana katika usiku kwa unavyo zidi usiku urefu wake. Na unatoa chenye sifa za kuonekana kihai katika kisicho kuwa na sifa za uhai, kama unavyo toa chenye kukosa uhai kutokana na kilicho hai, chenye kutamakani na sababu za uhai. Unampa neema zako kubwa umtakaye kwa mujibu wa mipango ya hikima zako. Hapana mchunguzi wa kukuhisabu Wewe. Huyo Mwenye shani hii haemewi na kumjaalia Mtume wake na awapendao, ubwana, na utawala, na utajiri, na wasaa, kama alivyo waahidi.