ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه‌ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس

شماره صفحه:close

external-link copy
109 : 5

۞ يَوۡمَ يَجۡمَعُ ٱللَّهُ ٱلرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَآ أُجِبۡتُمۡۖ قَالُواْ لَا عِلۡمَ لَنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّٰمُ ٱلۡغُيُوبِ

Na ikumbukeni, enyi watu, Siku ya Kiyama, siku Mwenyezi Mungu atakapo kuwakusanya Mitume, amani iwashukie, na awaulize kuhusu majibu ya watu wao waliyoyapata, pindi walipowalingania kwenye tawhīd (kumpwekesha Mwenyezi Mungu). Na wao watajibu, «Hatuna ujuzi, sababu hatuyajui yaliyomo ndani ya nyoyo za watu wala yale waliyoyazua baada yetu. Hakika yako wewe ni Mjuzi wa kila kitu kilichofichika na kilicho wazi. info
التفاسير:

external-link copy
110 : 5

إِذۡ قَالَ ٱللَّهُ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ ٱذۡكُرۡ نِعۡمَتِي عَلَيۡكَ وَعَلَىٰ وَٰلِدَتِكَ إِذۡ أَيَّدتُّكَ بِرُوحِ ٱلۡقُدُسِ تُكَلِّمُ ٱلنَّاسَ فِي ٱلۡمَهۡدِ وَكَهۡلٗاۖ وَإِذۡ عَلَّمۡتُكَ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَۖ وَإِذۡ تَخۡلُقُ مِنَ ٱلطِّينِ كَهَيۡـَٔةِ ٱلطَّيۡرِ بِإِذۡنِي فَتَنفُخُ فِيهَا فَتَكُونُ طَيۡرَۢا بِإِذۡنِيۖ وَتُبۡرِئُ ٱلۡأَكۡمَهَ وَٱلۡأَبۡرَصَ بِإِذۡنِيۖ وَإِذۡ تُخۡرِجُ ٱلۡمَوۡتَىٰ بِإِذۡنِيۖ وَإِذۡ كَفَفۡتُ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ عَنكَ إِذۡ جِئۡتَهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٞ

Atakaposema Mwenyezi Mungu, Siku ya Kiyama, «Ewe ‘Īsā mwana wa Maryam! Kumbuka neema yangu kwako, nilipokuumba bila ya baba, na kwa mamako, nilipomteua juu ya wanawake wa ulimwengu na nikamuepusha na hatia aliyobandikwa nayo.» Miongoni mwa neema hizi kwa ‘Īsā ni kwamba Mwenyezi Mungu Alimpa nguvu na Akamsaidia kwa Jibrili, amani imshukie, akasema na watu na yeye ni mchanga wa kunyonya kabla ya wakati wa kusema na akawaita wao kuja kwa Mwenyezi Mungu na yeye ni mkubwa, nguvu zake zimeshikana, na ubarobaro wake umekamilika, kwa wahyi wa tawhīd ambao Mwenyezi Mungu Alimletea. Na miongoni mwa hizo ni kwamba Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Alimfundisha kuandika na (kusoma) maandishi bila ya mwalimu, Alimpa nguvu ya kufahamu na kuelewa, Alimfundisha Taurati Aliyomteremshia Mūsā, amani imshukie, Injili Aliyomteremshia yeye ili kuwaongoza watu. Na miongoni mwa neema hizi ni kwamba yeye anasinyanga kwa udongo kama umbo la ndege na kisha anapuliza kwenye umbo hilo na likawa ni ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na miongoni mwazo ni kwamba yeye anamponyesha aliyezaliwa kipofu akawa anaona na anamponyesha mwenye mbalanga ikarudi ngozi yake kuwa na uzima kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na miongoni mwazo ni kwamba yeye anamuomba Mwenyezi Mungu Awahui wafu, na wakainuka kutoka kwenye makaburi yao wakiwa hai. Yote hayo ni kwa matakwa Mwenyezi Mungu , Aliyetukuka, na idhini Yake. Nayo ni miujiza yenye kushinda, inautilia nguvu unabii wa ‘Īsā, amani imshukie. Kisha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Anamkumbusha neema Yake kwake alipowazuia Wana wa Isrāīl walipotaka kumuua na akawajia wao na miujiza iliyo wazi yenye kuonyesha dalili za unabii wake. Hapo walisema waliokufuru kati yao, «Hakika haya aliyokuja nayo ‘Īsā, miongoni mwa dalili zilizo wazi, ni uchawi uliofichuka. info
التفاسير:

external-link copy
111 : 5

وَإِذۡ أَوۡحَيۡتُ إِلَى ٱلۡحَوَارِيِّـۧنَ أَنۡ ءَامِنُواْ بِي وَبِرَسُولِي قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَٱشۡهَدۡ بِأَنَّنَا مُسۡلِمُونَ

Na ukumbuke, ewe ‘Īsā, nilipotia ilhamu na msukumo katika nyoyo za watu, miongoni mwa wale waliosafiwa nawe, kuwafanya wauamini upweke wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na unabii wako, wakasema, «Tumeamini, ewe Mola wetu. Na ushuhudie kuwa sisi ni wenye kukunyenyekea na ni wenye kufuata kwa utiifu amri Yako. info
التفاسير:

external-link copy
112 : 5

إِذۡ قَالَ ٱلۡحَوَارِيُّونَ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ هَلۡ يَسۡتَطِيعُ رَبُّكَ أَن يُنَزِّلَ عَلَيۡنَا مَآئِدَةٗ مِّنَ ٱلسَّمَآءِۖ قَالَ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Na ukumbuke waliposema Ḥawāriyyūn (wasafiwa wa Nabii ‘Īsā kati ya wafuasi wake), «Ewe ‘Īsā mwana wa Maryam! Je, Anaweza Mola wako, ukimuomba, kututeremshia meza ya chakula kutoka mbinguni?» Jawabu yake ilikuwa ni kuwataka wao wajikinge na adhabu ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wakiwa ni wenye kuamini Imani ya kikweli. info
التفاسير:

external-link copy
113 : 5

قَالُواْ نُرِيدُ أَن نَّأۡكُلَ مِنۡهَا وَتَطۡمَئِنَّ قُلُوبُنَا وَنَعۡلَمَ أَن قَدۡ صَدَقۡتَنَا وَنَكُونَ عَلَيۡهَا مِنَ ٱلشَّٰهِدِينَ

Ḥawāriyyūn wakasema, «Tunataka kula kutoka kwenye meza hiyo, nyoyo zetu zipate kutulia kwa kuishuhudia, tupate kujua kwa yakini ukweli wako kuhusu unabii wako na tupate kuwa ni wenye kuishuhudia miujiza hii kwamba Mwenyezi Mungu Ameiteremsha iwe ni hoja kwetu juu ya upweke Wake na uwezo Wake kufanya Alitakalo na pia iwe ni hoja kwako juu ya ukweli kuhusu unabii wako.» info
التفاسير: