Na maombi yao kwenye Nyumba hii Tukufu (Al Kaaba) si chochote ila ni kupiga myunzi na makofi. Ilivyo kuwa hiyo ndiyo hali yenu, basi wacha mauti yakupateni, na yaonjeni katika uwanja wa vita, upate kubaidika (kuwa mbali) ushirikina kutokana na Al Kaaba. Na kuuliwa huko kwenu ni kwa sababu ya ukafiri wenu.