আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- আলী মুহছিন আল-বাৰওৱানী

পৃষ্ঠা নং:close

external-link copy
14 : 28

وَلَمَّا بَلَغَ أَشُدَّهُۥ وَٱسۡتَوَىٰٓ ءَاتَيۡنَٰهُ حُكۡمٗا وَعِلۡمٗاۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na Musa alipo fika utu-uzima baraabara, tulimpa akili na ilimu. Na hivi ndivyo tunavyo walipa walio wema. info

Na Musa alipo kwisha kuwa mtu mzima, na akakamilika, Mwenyezi Mungu alimpa hikima na ilimu. Na hisani kama hii tuliyo mpa Musa na mama yake, tunawapa wema wote kwa ajili ya wema wao.

التفاسير:

external-link copy
15 : 28

وَدَخَلَ ٱلۡمَدِينَةَ عَلَىٰ حِينِ غَفۡلَةٖ مِّنۡ أَهۡلِهَا فَوَجَدَ فِيهَا رَجُلَيۡنِ يَقۡتَتِلَانِ هَٰذَا مِن شِيعَتِهِۦ وَهَٰذَا مِنۡ عَدُوِّهِۦۖ فَٱسۡتَغَٰثَهُ ٱلَّذِي مِن شِيعَتِهِۦ عَلَى ٱلَّذِي مِنۡ عَدُوِّهِۦ فَوَكَزَهُۥ مُوسَىٰ فَقَضَىٰ عَلَيۡهِۖ قَالَ هَٰذَا مِنۡ عَمَلِ ٱلشَّيۡطَٰنِۖ إِنَّهُۥ عَدُوّٞ مُّضِلّٞ مُّبِينٞ

Na akaingia mjini wakati wa kughafilika wenyeji wake, na akakuta humo watu wawili wanapigana - mmoja ni katika wenzake, na mwengine katika maadui zake. Yule mwenzake alimtaka msaada kumpiga adui yake. Musa akampiga ngumi, akamuuwa. Akasema: Hiki ni kitendo cha Shet'ani; hakika yeye ni adui, mpotezaji dhaahiri. info

Musa akaingia mjini Misri wakati walipo kuwa watu wake wameghafilika. Akawakuta watu wawili wanapigana. Mmoja ni katika Wana wa Israili, na mwengine katika kaumu ya Firauni. Yule Muisraili akamtaka msaada kumpiga khasimu yake. Naye Musa akamsaidia. Akampiga konde yule khasimu, akamuuwa bila ya kukusudia. Musa akajuta na akasema: Hakika mimi kuja kufanya kitendo hichi ni kazi ya Shetani. Hakika Shetani ni adui aliye wazi kwa uadui na kupoteza.

التفاسير:

external-link copy
16 : 28

قَالَ رَبِّ إِنِّي ظَلَمۡتُ نَفۡسِي فَٱغۡفِرۡ لِي فَغَفَرَ لَهُۥٓۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimejidhulumu nafsi yangu; basi nisamehe. Akamsamehe; hakika Yeye ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu. info

Musa akasema kwa kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu na majuto: Ewe Mola wangu Mlezi! Mimi nimejidhulumu nafsi yangu kwa niliyo yatenda. Basi nighufirie kitendo changu hichi. Mwenyezi Mungu akamuitikia ombi lake na akamsamehe. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkuu wa kusamehe, Mkunjufu wa rehema.

التفاسير:

external-link copy
17 : 28

قَالَ رَبِّ بِمَآ أَنۡعَمۡتَ عَلَيَّ فَلَنۡ أَكُونَ ظَهِيرٗا لِّلۡمُجۡرِمِينَ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Kwa ulivyo nineemesha, basi mimi sitakuwa kabisa msaidizi wa wakosefu. info

Musa akasema kwa kunyenyekea: Ewe Mola wangu Mlezi! Kwa haki ya kunineemesha kwako kwa kunipa hikima, na ilimu, niwezeshe nitende kheri na yanayo faa. Ukiniwezesha hivyo basi kabisa sitakuwa msaidizi wa makafiri.

التفاسير:

external-link copy
18 : 28

فَأَصۡبَحَ فِي ٱلۡمَدِينَةِ خَآئِفٗا يَتَرَقَّبُ فَإِذَا ٱلَّذِي ٱسۡتَنصَرَهُۥ بِٱلۡأَمۡسِ يَسۡتَصۡرِخُهُۥۚ قَالَ لَهُۥ مُوسَىٰٓ إِنَّكَ لَغَوِيّٞ مُّبِينٞ

Akapambazukiwa mjini asubuhi naye ana khofu, akiangalia huku na huku. Mara yule yule aliye mtaka msaada jana akawa anampigia kelele amsaidie. Musa akamwambia: Hakika wewe ni mgomvi kweli kweli. info

Kulipo pambazuka asubuhi Musa alikuwapo mjini, Misri, naye yumo katika khofu, akitaraji kufikiwa na madhara kutokana na watu kwa sababu vile alivyo muuwa Mmisri. Akamwona yule Muisraili aliye mtaka msaada jana, naye akamtaka msaada mara ya pili katika ugomvi na Mmisri mwengine. Musa akamkemea kwa kumwambia: Hakika wewe mtu matata mno, na dhaahiri wewe ni mpotovu. Unafanya yale yale uliyo yafanya jana, na unaniita tena nikusaidie!

التفاسير:

external-link copy
19 : 28

فَلَمَّآ أَنۡ أَرَادَ أَن يَبۡطِشَ بِٱلَّذِي هُوَ عَدُوّٞ لَّهُمَا قَالَ يَٰمُوسَىٰٓ أَتُرِيدُ أَن تَقۡتُلَنِي كَمَا قَتَلۡتَ نَفۡسَۢا بِٱلۡأَمۡسِۖ إِن تُرِيدُ إِلَّآ أَن تَكُونَ جَبَّارٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا تُرِيدُ أَن تَكُونَ مِنَ ٱلۡمُصۡلِحِينَ

Basi alipo taka kumshika kwa nguvu yule aliye adui wao wote wawili, akasema: Ewe Musa! Unataka kuniuwa kama ulivyo muuwa mtu jana? Wewe hutaki ila kuwa jabari katika nchi, wala hutaki kuwa miongoni mwa wenye maslaha info

Na Musa alipo taka kumtumilia nguvu Mmisri, ambaye ni adui wao wote wawili; kwa sababu ya uadui huu, yule mtu alidhani kuwa Musa atamuuwa, basi akasema: Unataka kuniuwa kama ulivyo muuwa mtu jana? Wewe hutaki ila kuwa muasi tu katika nchi, wala hutaki kuwa miongoni wanao lingania maslaha na kheri.

التفاسير:

external-link copy
20 : 28

وَجَآءَ رَجُلٞ مِّنۡ أَقۡصَا ٱلۡمَدِينَةِ يَسۡعَىٰ قَالَ يَٰمُوسَىٰٓ إِنَّ ٱلۡمَلَأَ يَأۡتَمِرُونَ بِكَ لِيَقۡتُلُوكَ فَٱخۡرُجۡ إِنِّي لَكَ مِنَ ٱلنَّٰصِحِينَ

Na akaja mtu kutoka mwisho wa mji akipiga mbio, akasema: Ewe Musa! Wakubwa wanashauriana kukuuwa. Basi toka! Hakika mimi ni katika wanao kupa nasaha. info

Akaja mtu mmoja Muumini katika kaumu ya Firauni kutoka mwisho wa mji, ilipo enea khabari ya Musa kumuuwa Mmisri. Yule mtu akamwambia Musa kwamba watu wanapanga kutaka kumuuwa. Akamwambia: Toka mji, ukimbie usije ukauliwa! Hakika mimi ni katika wanao kupa nasaha.

التفاسير:

external-link copy
21 : 28

فَخَرَجَ مِنۡهَا خَآئِفٗا يَتَرَقَّبُۖ قَالَ رَبِّ نَجِّنِي مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّٰلِمِينَ

Basi akatoka, naye ana khofu, akiangalia huku na huku. Akasema: Mola wangu Mlezi! Niokoe na watu madhaalimu. info

Musa akautoka mji naye amejaa khofu wasije maadui wakamdhuru, akimnyenyekea Mwenyezi Mungu amwokoe na udhalimu wa makafiri.

التفاسير: