Walipo kuja wajumbe wetu, hao Malaika, kwa Lut' kwa sura ya vijana wazuri, Lut' aliungulika na akaudhika. Alihisi unyonge hana nguvu za kuwahami na hao watu wake, akawaonea dhiki kwa kuwaogopea ufisadi wa kaumu yake! Akasema: Hii leo ni siku ya karaha kubwa na machungu!