আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আৰু নাচিৰ খামীছ

পৃষ্ঠা নং:close

external-link copy
32 : 5

مِنۡ أَجۡلِ ذَٰلِكَ كَتَبۡنَا عَلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ أَنَّهُۥ مَن قَتَلَ نَفۡسَۢا بِغَيۡرِ نَفۡسٍ أَوۡ فَسَادٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ ٱلنَّاسَ جَمِيعٗا وَمَنۡ أَحۡيَاهَا فَكَأَنَّمَآ أَحۡيَا ٱلنَّاسَ جَمِيعٗاۚ وَلَقَدۡ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُنَا بِٱلۡبَيِّنَٰتِ ثُمَّ إِنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُم بَعۡدَ ذَٰلِكَ فِي ٱلۡأَرۡضِ لَمُسۡرِفُونَ

Kwa sababu ya uhalifu huu wa mauaji, tuliwaekea sheria Wana wa Isrāīl kwamba yoyote mwenye kumuua mtu pasi na sababu ya kulipiza kisasi au ya uharibifu katika ardhi, kwa aina yoyote kati ya aina za uharibifu zinazopelekea mauaji, kama ushirikina na uharamia, atakuwa ni kama kwamba amewaua watu wote kwa jinsi atakavyostahili mateso makubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kwamba yule atakayejizuia asiue mtu ambaye Mwenyezi Mungu Ameharamisha kuuawa, ni kama kwamba amewahuisha watu wote. Hivyo basi, kulinda heshima ya binadamu mmoja ni kulinda heshima ya binadamu wote. Hakika Mitume wetu waliwajia Wana wa Isrāīl kwa hoja na dalili juu ya usawa wa yale waliyowalingania kwayo ya kumuamini Mola wao na kuyatekeleza yale yaliyofanywa wajibu kwao na Mola wao. Kisha, wengi kati yao, baada ya kujiwa na Mitume ni wenye kupita mipaka ya Mwenyezi Mungu kwa kuyafanya yaliyoharamishwa na Mwenyezi Mungu na kuyaacha maamrisho yake. info
التفاسير:

external-link copy
33 : 5

إِنَّمَا جَزَٰٓؤُاْ ٱلَّذِينَ يُحَارِبُونَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَيَسۡعَوۡنَ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَسَادًا أَن يُقَتَّلُوٓاْ أَوۡ يُصَلَّبُوٓاْ أَوۡ تُقَطَّعَ أَيۡدِيهِمۡ وَأَرۡجُلُهُم مِّنۡ خِلَٰفٍ أَوۡ يُنفَوۡاْ مِنَ ٱلۡأَرۡضِۚ ذَٰلِكَ لَهُمۡ خِزۡيٞ فِي ٱلدُّنۡيَاۖ وَلَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ

Hakika malipo ya wale wanaompiga vita Mwenyezi Mungu na wanaojitokeza wazi kumfanyia uadui na kuzifanyia uadui hukumu zake na hukumu za Mtume Wake na kufanya uharibifu katika ardhi kwa kuwaua watu na kupora mali, ni wauawe au wasulubiwe pamoja na kuuawa (Kusululubiwa ni kufungwa mhalifu juu ya bao) au ukatwe mkono wa kulia wa mpiga vita na mguu wake wa kushoto. Iwapo hatatubu {kwa kuendelea na uharamia wake}, ukatwe mkono wake wa kushoto na mguu wa kulia, au wahamishwe wapelekwe mji usiokuwa wao, wafungwe kwenye jela ya mji huo mpaka iyonekane toba yao. Na haya ndiyo malipo Aliyoyaandika Mwenyezi Mungu kwa wenye kupiga vita; nayo ni unyonge wa duniani. Na huko Akhera itawapata adhabu kali iwapo hawatatubia. info
التفاسير:

external-link copy
34 : 5

إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ مِن قَبۡلِ أَن تَقۡدِرُواْ عَلَيۡهِمۡۖ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Lakini atakayekuja kati ya wale wanaopiga vita kabla hamjawatia mkononi na akaja akiwa mtiifu mwenye majuto, atafutiwa yale yaliyokuwa ni haki ya Mwenyezi Mungu. Na jueni, enyi Waumini, kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha kwa waja Wake, ni Mwenye kuwarehemu. info
التفاسير:

external-link copy
35 : 5

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱبۡتَغُوٓاْ إِلَيۡهِ ٱلۡوَسِيلَةَ وَجَٰهِدُواْ فِي سَبِيلِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ

Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Yake kivitendo, muogopeni Mwenyezi Mungu na mjisogeze karibu Kwake kwa kumtii na kufanya yanayomridhisha, na mpigane jihadi katika njia Yake ili mpate kufaulu kwa kuingia mabustani ya Pepo Yake. info
التفاسير:

external-link copy
36 : 5

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡ أَنَّ لَهُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا وَمِثۡلَهُۥ مَعَهُۥ لِيَفۡتَدُواْ بِهِۦ مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَا تُقُبِّلَ مِنۡهُمۡۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Hakika wale walioukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu na sheria Yake, lau walikuwa wao wamemiliki vyote vilivyoko ardhini na wakavimiliki vyingine mfano wake, na wakataka kuzikomboa nafsi zao, Siku ya Kiyama, na adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa hivyo walivyovimiliki, Mwenyezi Mungu Hangalikubali hilo. Na itawapata wao adhabu yenye kuumiza. info
التفاسير: