আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আৰু নাচিৰ খামীছ

পৃষ্ঠা নং:close

external-link copy
13 : 36

وَٱضۡرِبۡ لَهُم مَّثَلًا أَصۡحَٰبَ ٱلۡقَرۡيَةِ إِذۡ جَآءَهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Wapigie, ewe Mtume, washirikna wa watu wako wenye kukataa ulinganizi wako, mfano wa wao kuuzingatia nao ni hadithi ya watu wa kijiji walipoendewa na wajumbe. info
التفاسير:

external-link copy
14 : 36

إِذۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَيۡهِمُ ٱثۡنَيۡنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزۡنَا بِثَالِثٖ فَقَالُوٓاْ إِنَّآ إِلَيۡكُم مُّرۡسَلُونَ

Tulipowatumia wajumbe wawili wawalinganie kumuamini Mwenyezi Mungu na kuacha kumuabudu asiyekuwa Yeye. Watu wa kijiji wakawakanusha wajumbe wawili hao tukawatilia nguvu kwa mjumbe wa tatu. Basi hao wajumbe watatu walisema kuwaambia watu wa kijiji, «Hakika sisi kwenu nyinyi,enyi watu, tumetumwa.» info
التفاسير:

external-link copy
15 : 36

قَالُواْ مَآ أَنتُمۡ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَمَآ أَنزَلَ ٱلرَّحۡمَٰنُ مِن شَيۡءٍ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا تَكۡذِبُونَ

Watu wa kijiji wakasema kuwaambia wajumbe, «Hamkuwa nyinyi isipokuwa ni watu mfano wetu sisi, na Mwenyezi Mungu Hakuteremsha wahyi wowote. Na hamkuwa nyinyi isipokuwa mnasema urongo.» info
التفاسير:

external-link copy
16 : 36

قَالُواْ رَبُّنَا يَعۡلَمُ إِنَّآ إِلَيۡكُمۡ لَمُرۡسَلُونَ

Wajumbe wakasema kwa kutilia mkazo,»Mola wetu Aliyetutuma Anajua kwamba sisi, kwenu nyinyi, tumetumwa! info
التفاسير:

external-link copy
17 : 36

وَمَا عَلَيۡنَآ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na si juu yetu isipokuwa ni kufikisha ujumbe kwa uwazi, na hatuna mamlaka ya kuwafanya muongoke, kwani uongofu uko mikononi mwa Mwenyezi Mungu Peke Yake.» info
التفاسير:

external-link copy
18 : 36

قَالُوٓاْ إِنَّا تَطَيَّرۡنَا بِكُمۡۖ لَئِن لَّمۡ تَنتَهُواْ لَنَرۡجُمَنَّكُمۡ وَلَيَمَسَّنَّكُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٞ

Watu wa kijiji wakasema, «Sisi tumeingiliwa na kisirani kutokana na nyinyi, basi msipokomeka kutulingania,tutawaua kwa kuwapiga mawe na mtapata kutoka kwetu adhabu kali iumizayo.» info
التفاسير:

external-link copy
19 : 36

قَالُواْ طَٰٓئِرُكُم مَّعَكُمۡ أَئِن ذُكِّرۡتُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٞ مُّسۡرِفُونَ

Wajumbe wakasema, «Kisirani chenu na matendo yenu ya ushirikina na ya shari yako na nyinyi na yanarudishwa kwenu nyinyi. Je, nyinyi mkiwaidhiwa kwa jambo ambalo lina kheri kwenu mnajihisi mmeingiliwa na kisrani na mnatutisha kuwa mtatupiga mawe na kutuadhibu? Bali nyinyi ni watu ambao desturi yenu ni kupita kiasi katika uasi na ukanushaji. info
التفاسير:

external-link copy
20 : 36

وَجَآءَ مِنۡ أَقۡصَا ٱلۡمَدِينَةِ رَجُلٞ يَسۡعَىٰ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱتَّبِعُواْ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na akaja mtu kwa haraka kutoka mahali mbali mjini (Napo ni pale ilipojulikana kwamba watu wa kijiji wameazimia kuwaua wajumbe au kuwaadhibu) akasema, «Enyi watu wangu! Wafuateni wajumbe mlioletewa kutoka kwa Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
21 : 36

ٱتَّبِعُواْ مَن لَّا يَسۡـَٔلُكُمۡ أَجۡرٗا وَهُم مُّهۡتَدُونَ

Wafuateni wale wasiotaka mali kutoka kwenu kwa kufikisha Ujumbe na hali wao wako kwenye uongofu katika kile wanachowaitia cha kumuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake.» Katika hii kuna kueleza ubora wa mwenye kukimbilia kuamrisha mema na kukataza maovu. info
التفاسير:

external-link copy
22 : 36

وَمَالِيَ لَآ أَعۡبُدُ ٱلَّذِي فَطَرَنِي وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

«Na ni kitu gani kitakachonizuia kumuabudu Mwenyezi Mungu Aliyeniumba na Ambaye Kwake mtarejea nyote? info
التفاسير:

external-link copy
23 : 36

ءَأَتَّخِذُ مِن دُونِهِۦٓ ءَالِهَةً إِن يُرِدۡنِ ٱلرَّحۡمَٰنُ بِضُرّٖ لَّا تُغۡنِ عَنِّي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا يُنقِذُونِ

Je, niwaabudu waungu wengine wasiomiliki jambo lolote badala ya Mwenyezi Mungu? Iwapo Mwingi wa rehema Amenitakia mabaya, basi waungu hawamiliki kulikinga hilo wala kulizuia, wala hawawezi kuniokoa mimi na haya niliyonayo. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 36

إِنِّيٓ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

Mimi nifanyapo hivyo nitakuwa niko kwenya kosa lililo wazi lililojitokeza. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 36

إِنِّيٓ ءَامَنتُ بِرَبِّكُمۡ فَٱسۡمَعُونِ

Mimi nimemuamini Mola wenu, basi nisikilizeni nililowaambia na mnitii mimi kwa kuniamini.» Aliposema hilo, watu wake walimrukia wakamuua, na Mwenyezi Mungu Akamtia Peponi. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 36

قِيلَ ٱدۡخُلِ ٱلۡجَنَّةَۖ قَالَ يَٰلَيۡتَ قَوۡمِي يَعۡلَمُونَ

Aliambiwa baada ya kufa kwake, «Ingia Peponi,» kwa njia ya kutukuzwa. info
التفاسير:

external-link copy
27 : 36

بِمَا غَفَرَ لِي رَبِّي وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُكۡرَمِينَ

Akasema na yeye akiwa kwenye starehe na heshima, «Natamani watu wangu wangalijua vile Mola wangu Alivyonisamehe na kunikirimu kwa sababu ya kumuamini kwangu Mwenyezi Mungu na kusubiri kwangu juu ya kumtii Yeye na kuwafuata Mitume Wake mpaka nikauawa, ili nao wamuamini Mwenyezi Mungu na waingie Peponi kama mimi.» info
التفاسير: